Contact Us | FAQ | Mails | Complaints |

Public Health Education

FAHAMU KUHUSU UGONJWA WA HOMA YA INI

UGONJWA WA HOMA YA INI (HEPATITIS) : MAMBO MUHIMU YA KUFAHAMU

Ini ni kiungo muhimu sana ndani ya miili yetu, hufanya kazi zaidi ya 500 ; moja ya kazi ni kuchuja na kuondoa sumu kutoka kwenye damu.

Kutokana na sababu mbalimbali kama pombe iliyopita kiasi, sumu kwenye damu au maambukizi; ini hupata shida na kuvimba na kushindwa kufanya kazi vizuri. Hii hali huitwa HOMA YA INI au HEPATITIS.

Katika maeneo yetu, bara la Afrika maambukizi ya virusi wa Homa ya ini ndio sababu kuu ya shida kwenye ini. Virusi vya Homa ya ini vipo vya aina 5 (A,B,C,D,E).

Aina mbili za virusi (B na C ) ndio sababu kuu za ugonjwa wa homa ya ini na husambaa kupitia damu na majimaji ya mwili.

Homa ya ini ni sawa janga linaloua kimya kimya kulingana na takwimu za vifo za dunia inakadiriwa Kirusi cha homa ya ini aina ya B pekee huua watu 600,000 hivi kila mwaka.

Kwa wastani zaidi ya watu bilioni mbili, yaani, asilimia 33 hivi ya watu wote ulimwenguni, wameambukizwa virusi vya HBV, na wengi wao hupona baada ya miezi michache. Watu milioni 350 hivi huendelea kuwa na virusi hivyo mwilini, wengi huishi bila dalili na kuendelea kuambukiza watu wengine


NAMNA GANI UNAWEZA KUAMBUKIZWA VIRUSI VYA HOMA YA INI (B NA C)…….?

Virusi vya homa ya ini B na C husambaa kupitia damu, shahawa au maji maji mengine ya mwili.

Virusi hivi vina uwezo wa kusambaa na kuambukiza mtu mara 100 zaidi ya virusi vya UKIMWI.

Njia hizi husambaza virusi hivi vya homa ya ini..:

Kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto

➡️Mama aliye na maambukizi ya Hepatitis B kumuambukiza mtoto wakati wa kujifungua, iwapo hamna juhudi za kitiba za kuzuia maambukizi kuna uwezekano hadi asilimia 90 kwa mama kumuambukiza mtoto.

Kufanya mapenzi na mtu mwenye maambukizi ya virusi vya homa ya ini

Kuchangia vifaa vyenye ncha Kali kama sindano hasa kwa watumia madawa ya kulevya au wachora tattoo, miswaki

Kuongezewa damu ambayo ina maambukizi ya homa ya ini.

Virusi Vya Homa Ya Ini Vinaweza Ishi Nje Ya Mwili Kwa Muda Mrefu…

Tafiti zinaonyesha virusi vya homa ya ini vinaweza ishi nje ya mwili hadi kwa muda wa siku 7, bado vikiwa na uwezo wa kuambukiza mtu. Tafiti zimeonyesha hata iliyokauka huwa na uwezo wa kuambukiza virusi hivi.

Virusi Vya Homa Ya Ini Vinaweza Ishi Nje Ya Mwili Kwa Muda Mrefu…

Tafiti zinaonyesha virusi vya homa ya ini vinaweza ishi nje ya mwili hadi kwa muda wa siku 7, bado vikiwa na uwezo wa kuambukiza mtu. Tafiti zimeonyesha hata iliyokauka huwa na uwezo wa kuambukiza virusi hivi.


NB : Iwapo kuna damu imemwagika inatakiwa isafishwe na chlorine au spirit ili kuua virusi

NANI YUPO KATIKA HATARI ZAIDI YA KUPATA MAAMBUKIZI YA VIRUSI VYA HOMA YA INI?

° Watoto wachanga waliozaliwa na mama aliye na maambukizi ya virusi vya homa ya ini

° Watu wanaofanya biashara ya ngono

°Wanaume wanaofanya mapenzi na wanaume wenzao

°Watu wanaojidunga dawa za kulevya

° Mtu mwenye mpenzi ambaye anaishi na maambukizi ya virusi vya homa ya ini

° Wafanyakazi wa sekta ya Afya

° Watu wa familia wenye ndugu anayeishi na maambukizi ya kudumu ya virusi vya homa ya ini

°Wagonjwa wa figo wanaotumia huduma za kusafisha damu (dialysis)

UGONJWA WA VIRUSI VYA HOMA YA INI HUJA NA DALILI MBALIMBALI…..

Dalili Za Muda Mfupi (Acute Hepatitis)

➡️ Dalili hizi za mwanzo hutokea ndani ya miezi 6 baada kuambukizwa virusi vya homa ya ini, hutokea kwa baadhi ya watu hazitokei kwa kila mtu.

Mgonjwa mwenye maambukizi ya virusi vya homa ya ini hujiskia kuumwa

Hupoteza hamu ya kula

Kichefuchefu na kutapika

Mwili kuuma

Mkojo kuwa na rangi iliyokolea kama Coca-Cola

Kupata manjano kwenye macho, vinganja vya mikono/kucha au mwili mzima.


Kuna kundi dogo la wagonjwa wa homa ya ini hupata ugonjwa mkali wa ini na kusababisha ini kushindwa kabisa kufanya kazi pia huweza kusababisha kifo. Hii hatua huitwa “fulminant liver failure”.

Maambukizi Ya Kudumu Ya Virusi Vya Homa Ya Ini (Chronic Hepatitis)

Watu wenye maambukizi ya kudumu ya virusi vya homa ya ini mara nyingi huwa hawana dalili, kadri muda unavyoenda virusi husababisha ini kusinyaa (cirrhosis) na kushindwa kufanya kazi vyema.


Pia Maambukizi ya virusi vya homa ya ini huchangia pia kupata Saratani ya ini.


Kwa nini ni muhimu kupima ili kujua kama una maambukizi ya virusi vya homa ya ini? ….

Watu wengi huishi na maambukizi ya virusi vya homa ya ini bila kufahamu. Kwa kawaida katika kipindi fulani cha maisha mtu 1 kati ya watu 3 huambukizwa virusi vya homa ya ini. Baada ya kuambukizwa, kuna kundi la watu hubaki na maambukizi ya kudumu ya virusi vya homa ya ini ambayo huwa hayana dalili yoyote na kuendelea kuua ini kimyakimya. Dalili huja kuonekana waziwazi miaka mingi baada ya mtu kuambukizwa. Huonekana wakati tayari ini limenyauka au lina kansa.

Hivyo Mtu aliye na maambukizi ya kudumu ya virusi vya homa ya ini aina B akianza matibabu mapema, anaweza kuzuia ini lake lisiharibike sana. Pia kwa wenye maambukizi ya virusi aina C matibabu ya dawa wiki 12 humaliza virusi vyote.

NANI ANAHITAJI KUPIMWA MAAMBUKIZI YA HOMA YA INI?

Watu kutoka makundi yafuatayo ni sharti kupimwa kama wana maambukizi ya virusi wa homa ya ini……

Watu wanaoishi kwenye maeneo yenye maambukizi ya virusi vya homa ya ini kwa zaidi ya asilimia 2. -Tanzania ni moja ya nchi zenye kiwango cha maambukizi ya virusi vya homa ya ini kwa wastani wa 5% hivyo watanzania wote ni muhimu kupima

Watu wote wanaotumia dawa za kulevya na kujidunga

Wafanyakazi katika sekta ya afya

Watu wote wanaoishi na maambukizi ya virusi vya UKIMWI

Watu wote ndani ya familia wanaoshi na ndugu aliyeambukizwa virusi vya homa ya ini

Watu wote wanaotumia dawa za kufubaza kinga ya mwili (immunosuppressive therapy)

Watu wote wenye ugonjwa wa figo wanahitaji kuanza dialysis

Kina mama wajawazito wote

Wanaume wanaofanya mapenzi na wanaume wenzao.

UGONJWA WA HOMA YA INI HUWA NA MATOKEO MABAYA…..

Kwa wastani watu 25 kati ya 100 walioambukizwa virusi vya homa ya ini wakiwa watoto na 15 kati ya 100 waliopata maambukizi ya kudumu ya homa ya ini baada ya utoto hufariki wakiwa na umri mdogo kwa ugonjwa wa ini (ini kushindwa kufanya kazi) au saratani ya ini.

CHANJO YA DHIDI YA VIRUSI VYA HOMA YA INI


Chanjo dhidi ya homa ya ini hutolewa kwa watoto wote kama ilivyo kwenye mpango wa chanjo wa Taifa, pia hutolewa kwa watu wazima ambao hawajawahi kupata chanjo.

Chanjo hutolewa kwa njia ya sindano, ambapo huwa ni sindano 3; sindano ya kwanza hutolewa baada ya kupimwa kujua kama hauna maambukizi tayari, sindano ya pili hutolewa baada ya mwezi mmoja na sindano ya 3 baada ya miezi 6.

Makundi ambayo ni lazima kupatiwa chanjo ya homa ya ini

Watoto wote

Watu wote wanaotumia dawa za kulevya na kujifungua

Watu wote wanaoishi na maambukizi ya virusi vya UKIMWI

Watu wote ndani ya familia wanaoshi na ndugu aliyeambukizwa virusi vya homa ya ini

Watu wote wanaotumia dawa za kufubaza kinga ya mwili (immunosuppressive therapy)

Wanaume wanaofanya mapenzi na wanaume wenzao

Watu wote wanaoufanya biashara ya ngono

Watu wote ambao wana mpenzi zaidi ya mmoja ndani ya miezi 6

Watu wenye maradhi ya kudumu ya ini

Watu wengine wote wanahitaji KUJIKINGA dhidi ya virusi vya homa ya ini

read more
FAHAMU KUHUSU UGONJWA WA EBOLA

FAHAMU KUHUSU HOMA YA EBOLA

Ugonjwa wa Homa ya Ebola ni ugonjwa wa hatari unaosababishwa na virusi vya ebola. Ugonjwa huu ni miongoni mwa magonjwa ya milipuko yajulikanayo kama homa za virusi vinavyo sababisha kutoka damu mwilini.

Kuna aina tano za virusi vinavyosababisha ugonjwa wa ebola kama ifuatavyo; Zaire ebola virus, Sudan ebolavirus,Taï Forest ebolavirus, na Bundibugyo ebolavirus).Hivi vinasababisha ugonjwa wa Homa ya Ebola kwa binadamu.Kirusi cha tano kinaitwa Reston ebolavirus ambacho husababisha ugonjwa wa Ebola kwa wanyama peke yake

Ugonjwa huu kwa asili huanzia kwa wanyama kama vile nyani, kima sokwe na popo. Ugonjwa wa homa ya ebola huambukizwa kutoka kwa wanyama kwenda kwa binadamu au binadamu kwa binadamu mwingine kwa njia ya haraka.


Jinsi ya ugonjwa wa homa ya ebola unavyoambukizwa toka kwa wanyama kwenda kwa binadamu

Binadamu anapata virusi vya ugonjwa wa homa ya Ebola kwa kula au kugusa viungo na majimaji ya wanyama pori wenye maambukizi ya ugonjwa huo.

Jinsi ya ugonjwa wa ebola unavyoambukizwa miongoni mwa jamii

  • Kugusa majimaji ya mwili kama vile damu, matapishi, jasho, mate, machozi, mkojo au kinyesi kutoka kwa mtu aliyeambukizwa na ugonjwa huo
  • Kugusa au kuosha maiti ya mtu aliyeku fa kwa ugonjwa wa ebola
  • Kugusa vyombo na nguo zilizotumiwa na mtu mwenye maambukizi ya ebola
  • Kutumia vifaa vilivyotumika kum hudumia mgonjwa wa homa ya Ebola kama vile Sindano au Nyembe
  • Kujamiana na mtu mwenye maambukizi ya virusi vya Ebola

Ugonjwa huu hauenezwi kwa njia ya Hewa,Maji au Chakula

 

  Dalili za ugonjwa wa homa ya ebola                      

Dalili za ugonjwa wa homa ya ebola huanza kujitokeza kwa mtu aliyeambukizwa na virusi hivi kuanzia siku 2 hadi 21 tangu kupata maambukizi. Dalili hizo ni pamoja na:

  • Homa kali
  • Kulegea kwa mwili
  • Maumivu ya misuli
  • Kuumwa kichwa na vidonda kooni
  • Mara nyingi dalili hizo hufuatiwa na kutapika, kuharisha na vipele vya ngozi
  • Kwa baadhi ya wagonjwa kutokwa na virusi
  • damu hutoka sehemu za wazi za mwili kama vile kwenye macho, pua, masikio, mdomo na njia za haja ndogo na kubwa

    Matibabu                                                                 

Ugonjwa wa homa ya ebola hauna tiba maalum wala chanjo, hata hivyo mgonjwa hutibiwa kulingana na dalili zitakazo ambatana na ugonjwa huo. Kuna uwezekano mkubwa wa  kuepuka mgonjwa kupoteza maisha iwapo mgonjwa huyo hatawahi kupata huduma stahiki.

  Jinsi ya kujikinga na ugonjwa wa homa ya ebola Ugonjwa wa homa ya ebola unaweza kuzuilika iwapo tutazingatia yafuatayo;

  • Epuka kugusa damu, matapishi, kamasi, mate, machozi, mkojo, kinyesi na majimaji yanayotoka kwenye mwili wa mtu mwenye dalili za ugonjwa wa homa ya ebola.
  • Epuka kugusa au kuosha maiti ya mtu aliyekufa akiwa na dalili za ugonjwa wa homa ya ebola, toa taarifa kwenye kituo cha kutolea huduma za afya kwa ushauri.
  • Epuka kutumia sindano,Kiwembe,m kasi,nguo, matandiko, kitanda, godoro na vyombo vilivyotumika na mtu mwenye dalili za ugonjwa wa homa ya ebola
  • Epuka kukutana kimwili na mtu mwenye dalili za ugonjwa wa homa ya Ebola
  • Epuka kugusa wanyama kama vile popo, nyani sokwe, tumbili na swala au mizoga ya wanyama.
  • Zingatia ushauri na maelekezo yanayotolewa na wataalamu wa afya na viongozi wa serikali.
  • Wahi kituo cha kutolea huduma za afya unapohisi mojawapo ya dalili za ugonjwa wa ebola
  • Toa taarifa mapema kwenye kituo cha huduma za afya au kwa viongozi wa serikali ya mtaa, kijiji au kata mara uonapo mtu mwenye dalili za ugon jwa wa ebola.
read more
FAHAMU JINSI YA KUJIKINGA NA VIRUSI VYA CORONA

VIRUSI VYA CORONA NI NINI?

Kuna vimelea vingi vya magonjwa duniani kote kama Bakteria , Virusi ,Fangi ,Protozoa na Parasaiti

Aghalabu katika makundi yote haya Kuna aina za vimelea ambavyo huwa hatarishi mno na huua haraka wanyama wanyonyeshao na ndege (ambayo ndio makundi yanayoathiriwa mno na vimelea hivi)

Milipuko ya tauni ,kipindupindu(cholera) ,ebola ,malaria Homa ya ini (hasa hepatitis B ) ,Ukimwi (HIV) na homa za mafua vimekuwa tishio kwa miaka mingi nyuma na hivi karibuni na kuua watu wengi mno.

Barani Afrika bado tunao upungufu mkubwa was kupata taarifa za kutosha kuhusu mazingira ,mwingiliano wa viumbe hai na Afya kwa ujumla.

Jamii kubwa barani Afrika na nchi nyinginezo za ulimwengu wa tatu ni jamii ya watu wenye Elimu ya chini mno kuweza kuelewa kwa undani taarifa hizi na na hivyo kupelekea kuathirika mno na magonjwa.

Kuna makundi mengi mno ya virusi duniani kote ,na mengi ya makundi hayo hayana tiba maalumu japo Kuna maendeleo makubwa ya utengenezaji na uboreshaji wa chanjo ,madawa ya kupunguza makali ya maambukizi na kuzaliana pamoja mbinu mbalimbali za kujikinga.

mambo machache kuhusu virusi vya Corona .Ambavyo pia vina makundi manne ya alpha,beta,gamma na Delta 

Jina *"coronavirus"* limetokana na neno la Kilatini na *κορώνη* au *korṓnē,* ikimaanisha *taji* (neno la kiingerza *Crown*

Hii NI kwa sababu ya muonekano wa tabia wa umbo la kirusi hiki ukitumia darubini ya elektroni, ambayo itakuonyesha umbo kama la *taji ya kifalme* au alama ya jua.

Watu mamia kwa mamia wanazidi kufa huko China na historia ya Muda mrefu ya mlipuko wa virusi vya corona huko mashariki ya kati.

Virusi vya Corona ni kundi la virusi ambavyo husababisha magonjwa katika mamalia na ndege.

Kwa wanadamu, virusi hivi husababisha magonjwa ya kupumua ambayo kitaalamu huitwa Systemic Acute Respiratory Syndromes (SARS) aina mojawapo ya Pneumonia ambayo kwa kawaida hupelekea mgonjwa kupumua kwa shida sana na kukosa nguvu , kukohoa na homa Kali Coronaviruses husababisha homa Kali na uvimbe katika koo, kwa wanadamu hasa wakati wa msimu wa baridi.

Coronaviruses wanaaminika kusababisha asilimia kubwa ya homa zote za kawaida kwa watu wazima na watoto.

Virusi hivi vina protini zinazoweza kuvisaidia kushikilia na kuishi kwa kutegemea seli za viumbe hai wengine na gamba maalumu linaloathiri kemikali/enzyme za Figo na kupelekea kuharibika haraka kwa Figo na viungo vingine hasa kwa wagonjwa wenye Kinga ndogo ya mwili.

SARS huweza kupona ndani ya kipindi kifupi ,lakini Muda mwingine yanaweza kuwa mabaya na kupelekea kifo.

Katika ng'ombe na nguruwe (Feline Coronavirus)zinaweza kusababisha kuhara, wakati katika kuku zinaweza kusababisha ugonjwa wa kupumua kwa shida

Maambukizi ya Corona yaliiyotangazwa sana ya binadamu baada ya kugunduliwa ni Yale ya mnamo mwaka 2003, SARS-CoV2003

Maambukizi haya ya tofauti husababisha mkusanyiko wa magonjwa ya kupumua kwa shida na ni ya kipekee kwani hupelekea matatizo ya kupumua ya juu kwenye koo la hewa na ya chini kwenye mapafu

Mpaka Sasa Kuna aina saba za Corona wanaathiri binadamu 

  • Human Coronavirus 229E (HCoV-229E)
  • Human Coronavirus OC43 (HCoV-OC43)
  • SARS-CoV
  • Human Coronavirus NL63 (HCoV-NL63, coronavirus mpya ya Haven huko )
  • Human Coronavirus HKU1
  • Middle East Respiratory syndrome Coronavirus MERS-Cov
  • Novel coronavirus (2019-nCoV)


Novel coronavirus (2019-nCoV)

inajulikana pia kama *Wuhan pneumonia* au Wuhan coronavirus kwa sababu imegunduliwa katika Jimbo la Wuhan huko China na kutambuliwa na mamlaka huko Wuhan, Hubei, Uchina, kama sababu ya mlipuko wa coronavirus unaoendelea wa 2019-20.

Jina hili linatokana na ugunduzi mpya, na Imegunduliwa karibuni tu Disemba mwaka jana na ndio imekuwa tishio mpaka Sasa huko china.

Novel Coronavirus ya 2019 (2019-nCoV) ni virusi vya kuambukiza ambavyo husababisha maambukizo ya kupumua na tayari tafiti zimeonyesha ushahidi wa maambukizi kati ya Mtu na mtu kama ilivyothibitishwa huko Guangdong, china, Januari 20, 2020.

Kuna ripoti ya uchunguzi wa awali inaonesha kwamba maambukizi haya kutokea kwa vyakula wa baharini ,nyoka na popo ambayo ni vyakula vya kitamaduni vya kichina na tafiti nyingi zinaonesha Coronavirus kuishi ndani ya viumbe hawa pia. Virusi hivi pia hukaa ndani ya paka ,nguruwe na hata ngamia.

Ulinganishoo wa maumbile kati ya virusi hivi na sampuli zingine za virusi zilizopo zimeonyesha kufanana kwa SARS-CoV (79.5%)

Mlipuko wa kwanza Virusi umegunduliwa huko Wuhan, Uchina, katikati ya Desemba 2019 na baadaye vilienea kwa kasi katika majimbo mengine ya Bara la China na nchi zingine, pamoja na Thailand, Japan, Taiwan, Korea Kusini, Australia, Ufaransa, na Amerika.

Kufikia tarehe 27 Januari 2020, tayari kuna kesi 2,006 zilizothibitishwa za maambukizi ambapo 1825 wako ndani ya China Bara. Idadi ya vifo mpaka Sasa imefikia 81 kutoka tar 27 Januari 2020.

kuenea kwake

Coronavirus ni ugojwa unaoambukiwa Kwanza kutoka kwa wanyama au kwa kitaalamu huitwa ZOONOSTIC INFECTIONS na mtu aliyeambukizwa huweza kueneza kwa wengine kwa njia ya hewa pale akikohoa ,kupumua au kupiga chafya. 

Dalili 

Kuna dalili kuu nne za awali ambazo ni

  • Uchovu,
  • kikohozi kikavu,
  • upungufu wa pumzi, na
  • shida ya kupumua.

Kesi za maambukizo mazito zinaweza kupelekea pneumonia, kuharibika kwa figo, na hata kifo. Katika taarifa iliyotolewa tarehe 23 Januari 2020, Mkurugenzi Mkuu wa WHO Tedros Adhanom alisema kwamba robo ya wale walioambukizwa walipatwa ghafula na kwamba wengi wa wale waliokufa walikuwa na hali zingine kama shinikizo la damu, ugonjwa wa sukari au ugonjwa wa moyo na mishipa ambayo ilisababisha kinga yao kuwa chini kuweza kupambana na maambuki haya.

Utafiti wa wagonjwa 41 wa kwanza waliolazwa katika hospitali za Wuhan na kesi zilizothibitishwa ziliripoti kuwa wagonjwa wengi walikuwa na afya kabla ya kuambukizwa ugonjwa huo, na kwamba zaidi ya robo ya watu wazima wenye afya walihitaji huduma ya uangalizi wa karibu. Kati ya idadi kubwa ya wale walielazwa hospitalini, walikuwa na idadi ndogo ya seli nyeupe za damu na kiwango cha chini cha damu.

Matibabu .

Mpaka Sasa Hakuna matibabu maalumu ya Coronaviruses zaidi ya kutibu dalili na matatizo yasabishwayo na Virusi hawa kama Homa ,maumivu ya viungo ,hewa ya oksijeni na dawa za kusaidia upumuaji .

Kuna tafiti nyingi bado zinaendelea mpaka sasa.

read more